
Mathayo 6:19-21
Nimewekeza hazina yangu juu mbinguni,
Nimewekeza kwa Mungu wangu.
Nimeyatoa maisha yangu niwe dhabihu,
Nimejitoa kwa Mungu wangu.
Mambo ya dunia ni ya kitambo tu,
Ya haribika Tena yapita.
Hakita bakia kitu kwa dunia,
Vya haribika tena vya pita.
Nimewekeza hazina yangu juu mbinguni,
Nimewekeza kwa Mungu wangu.
Nimeyatoa maisha yangu niwe dhabihu,
Nimejitoa kwa Mungu wangu.
Mimi nita-jisifia nini cha ulimwengu,
Hata kifanye nimkosee Mungu.
Vyote ni kwa mapenzi ya Mungu,
Si kwa nguvu zangu..
Nataka nifae mbele za Mungu .
Kwake Mungu hakuna nondo madumadu na parare,
Mimi nataka nifae mbele za Mungu.
Huko iliko hazina yangu, Ndiko uliko moyo wangu,
Mimi nataka nifae mbele za Mungu.
Wekeni hazina mbinguni,
Haita pungua akiba yenu Mbinguni kwa Baba
Jifanyieni mifuko, isiyo chakaa kabisa,
Mbinguni kwa Baba.
Audio Recorded by: Frester's Record
Graphics By: Titus Alfred
Contacts:
Email: neemagospelchoir@gmail.com
Phone: +255 (0) 766 777 288
Instagram: neema_gospel_choir
Facebook: Neema Gospel Choir
Twitter: Neema Gospel Choir
Telegram: Neema Gospel Choir